Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mheshimiwa Patrobas Katambi ameongoza kikao kazi cha kupitia Rasimu ya Hotuba ya wizara hiyo ambapo kikao hicho kilipitia Makadirio na Matumizi ya Fedha kwa mwaka 2026/2027 ambapo inatarajiwa kuwasilishwa tarehe 25/5/2026 Bungeni, jijini Dodoma.
Kikao kazi hicho kilihudhuriwa pia na Naibu Waziri,Mheshimiwa Ayoub Mohammed Mahmoud,Katibu Mkuu,Ally Senga Gugu, Naibu Katibu Mkuu,Dkt. Maduhu Kazi, Menejimenti ya Wizara, Wawakilishi wa Wakuu wa Vyombo vya Usalama vilivyopo chini ya wizara, ikiwemo Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Idara ya Uhaamiaji, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA) na Maafisa Waandamizi kutoka wizarani na kwenye vyombo vya usalama.
Kikao kazi hicho kimefanyika Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,jijini Dodoma.









0 Comments