Ticker

6/recent/ticker-posts

DKT.GWAJIMA AFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI WA SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UBUNIFU WA UGANDA.


******************************

Na.WAMJW- DAR

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima leo amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu wa Uganda Dkt. Monica Musenero Masanza aliyeambatana na Wataalamu kutoka Wizara hiyo ya Uganda.

Katika Mkutano huo kwa pamoja wamekubaliana kushirikiana katika mapambano dhidi ya magonjwa mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa UVIKO-19 ili kulinda afya za wananchi wa Tanzania na Uganda.

Aidha, Dkt. Gwajima amemhakikishia utayari wa Wizara yake kushirikiana na Wizara yake nchini Uganda ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi na kuleta matokeo chanya katika Sekta ya Afya baina ya nchi hizo.

Naye Waziri wa Sayansi, Teknlojia na Ubunifu nchini Uganda Dkt. Monica Musenero amesema, Uganda iko tayari kushirikiana na Tanzania katika katika mapambano dhidi ya magonjwa mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa UVIKO-19.

Kikao hicho kimefanyika katika kituo cha mikutano ya kimataifa cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Post a Comment

0 Comments