Ticker

6/recent/ticker-posts

BALOZI MBAROUK AONGOZA WAOMBOLEZAJI KATIKA KUAGA MWILI WA BALOZI EDWIN RUTAGERUKA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) akiongoza waombolezaji katika kuaga mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasi ya Uchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Marehemu Balozi Edwin Rutageruka katika kijiji cha Musibuka, Wilayani Misenyi Mkoani Kagera.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) akitoa salamu za mwisho kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasi ya Uchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Marehemu Balozi Edwin Rutageruka katika mazishi yaliyofanyika kijiji cha Musibuka, Wilayani Misenyi Mkoani Kagera.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine akitoa salamu za rambirambi kwa ndugu na jamaa wa familia ya marehemu Balozi Edwin Rutageruka wakati wa mazishi yaliyofanyika katika kijiji cha Musibuka Wilayani Misenyi Mkoani Kagera
Sehemu ya Waombolezaji wakiwa msibani

Askofu msaidizi wa Jimbo katoliki la Bukoba Mhashamu Methodius Kilaini akiongoza ibada ya mazishi ya aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasi ya Uchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Marehemu Balozi Edwin Rutageruka katika mazishi yaliyofanyika jana kijijini kwake Musibuka, Wilayani Misenyi Mkoani Kagera
Askofu msaidizi wa Jimbo katoliki la Bukoba Mhashamu Methodius Kilaini akisimika msalaba kwenye kaburi la aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasi ya Uchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Marehemu Balozi Edwin Rutageruka
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) pamoja na mume wake wakiweka shada la maua kwenye kaburi la Balozi Edwin Rutageruka.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akiweka taji kwenye kaburi la Balozi Edwin Rutageruka.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Idara na Vitengo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiweka mashada ya maua kwenye kaburi la Balozi Edwin Rutageruka kwa niaba ya Menejimenti ya Wizara hiyo.
Naibu Waziri Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara wakiwa katika picha ya pamoja kwenye kaburi la Marehemu Balozi Edwin Rutageruka mara baada ya maziko ya Balozi Edwin Rutegaruka

Post a Comment

0 Comments