Ticker

6/recent/ticker-posts

MAYELE APIGA HAT- TRICK, YANGA SC IKIFUZU HATUA INAYOFUATA CAFSC



***********************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KLABU ya Yanga imefuzu hatua inayofuata klabu bingwa Afrika baada ya kufanikiwa kuwachapa jumla ya mabao 9-0 timu ya Zalan Fc ya nchini Sudan ya Kusini.

Mechi ya kwanza Yanga ilifanikiwa kuwachapa mabao 4-0, wakati mechi ya pilia mabyo imepigwa leo katika dimba la Benjamini Mkapa imeilaza kwa mabao matano na kufanya jumla ya kuwa na mabao 9-0.

Ni Fiston Kalala Mayele amefanikiwa kufunga mabao matatu tena yaani Hat Trick baada ya mechi ya kwanza kufanya hivyo.

Mabao mengine ya Yanga yamewekwa kimyani na Farid Mussa na Aziz Ki .

Post a Comment

0 Comments