Ticker

6/recent/ticker-posts

TANZANIA NA DRC ZAKUTANA DAR KUJADILI BIASHARA NA UWEKEZAJI


Mkurugenzi wa Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Naimi Aziz akiwakaribisha Makatibu Wakuu wa Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Balozi Joseph Sokoine na Mhe. Zacharie Tshimbinda Bilolo kusoma hotuba za ufunguzi za Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC.
Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akipitia hotuba yake ya ufunguzi ya Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC.
Mkurugenzi wa Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Naimi Aziz akifafanua jambo kwa viongozi kuhusu Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC.
Sehemu ya Ujumbe wa DRC unaoshiriki Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC.
Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC ngazi ya wataalam unaendelea jijini Dar Es Salaam.


Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akizungumza jambo na Konseli Mkuu wa Tanzania, Lubumbashi, Bw. Selestine Kakere kabla ya ufunguzi wa Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC.
Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mtangamano wa Kikanda na Nchi zinazongumza Kifaransa wa DRC, Mhe. Zacharie Tshimbinda Bilolo wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Tanzania na DRC wanaoshiriki Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC.

Post a Comment

0 Comments