Ticker

6/recent/ticker-posts

UZINDUZI WA WIKI YA UTAFITI NA UBUNIFU KATIKA CHUO CHA DUCE

Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mwanahamisi Munkunda akifurahi jambo na Naibu Mkuu wa DUCE (Mipango, Fedha na Menejimenti) Prof. Method Samwel wakati akikagua baadhi bunifu katika uzinduzi wa Wiki ya Nane ya Utafiti na Ubunifu ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), yaliyofanyika chuoni hapo Jijini Dar es Salaam

**********************

Watafiti wa kitaaluma wamepewa changamoto ya kuja na kazi za utafiti ambazo zina athari ya moja kwa moja kwa maisha ya watu kupitia kutoa suluhisho kwa shida zinazowaathiri.

Wito huo umetolewa hivi karibuni na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mwanahamisi Munkunda wakati wa uzinduzi wa Wiki ya nane ya Utafiti na Ubunifu ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) inayotarajiwa kufikia kilele leo.

Katika hotuba yake katika hafla iliyofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DUCE) kampasi kuu ya jijini hapa, alisisitiza umuhimu wa kuzingatia sana tafiti zinazosaidia kutokomeza matatizo yanayowakabili watu na kufanya maisha yao kuwa bora.

“Nimefurahi kuona DUCE inachukua nafasi kubwa katika kufanya kazi nzuri za utafiti zikiwemo nilizoziona za kuhifadhi mazingira ambayo ni muhimu sana kwa maisha yetu ya kila siku.

“Pia, nimefurahishwa kujua kuwa mna uwezo wa kuzalisha bidhaa za ziada ambazo ni muhimu kwa maendeleo ya bidhaa mbalimbali ikiwamo kulinda mazingira,” alisema.

Zaidi ya hayo, DC huyo alibainisha kuwa alifurahi pia kuona kwamba baadhi ya watafiti walitengeneza nyenzo za kuzuia mbu wakisema ni muhimu kwa ajili ya kuimarisha afya za watu kwani hawatashambuliwa na mbu ambao hatimaye husababisha malaria.

Kisha akatangaza kuwa yuko tayari kuwa balozi wa DUCE haswa ili kukuza kazi mbalimbali za utafiti ambazo taasisi hiyo hutoa kila mwaka.

Aidha, Bi. Munkunda alipongeza ushirikiano mzuri uliopo kati ya taasisi hiyo na jamii akisema tangu alipokuwa DC wa Tememe, hajawahi kusikia malalamiko yoyote kuhusu DUCE.

Awali Naibu Mkuu wa DUCE (Mipango, Fedha na Menejimenti) Prof. Method Samwel alibainisha kuwa mwaka huu, kuna kazi 30 za utafiti zilizofanywa na wahadhiri huku wanafunzi wakionyesha kazi 10.

“Mbali na kufanya utafiti na ubunifu, wahadhiri wetu pia wanafundisha wanafunzi jinsi wanavyoweza kufanya tafiti muhimu ili ziweze kutumika kwa matumizi ya binadamu,” alisema.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mwanahamisi Munkunda akitazama bunifu zilizofanywa na DUCE katika Uzinduzi wa Wiki ya Nane ya Utafiti na Ubunifu ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), yaliyofanyika chuoni hapo Jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mwanahamisi Munkunda akimsikiliza mbunifu wa DUCE katika wa uzinduzi wa Wiki ya Nane ya Utafiti na Ubunifu ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), yaliyofanyika chuoni hapo Jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mwanahamisi Munkunda akizungumza katika uzinduzi wa Wiki ya Nane ya Utafiti na Ubunifu ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), yaliyofanyika chuoni hapo Jijini Dar es Salaam
Naibu Mkuu wa DUCE (Mipango, Fedha na Menejimenti) Prof. Method Samwel akizungumza katika uzinduzi wa Wiki ya Nane ya Utafiti na Ubunifu ya Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE), yaliyofanyika chuoni hapo Jijini Dar es Salaam

Post a Comment

0 Comments