Ticker

6/recent/ticker-posts

WALE WAPENZI WA SIMU BEI KITONGA, ITEL WANA JAMBO LENU

Ni vigumu kuamini kuwa Tsh.160,000 inaweza kukupatia simu yenye uwezo wa 4G, betri kubwa 5000mAh linalodumu muda mrefu, kioo kikubwa kwa wale wapenda movies za simu na muonekano mzuri sana.

Kampuni inayotamba nchina Tanzania kwa kuuza simu zenye ubora na kujali kipato cha mtu wa kati itel inatarajia kuachia simu yake mpya katika toleo la “A” series kwa jina la Itel A60 yenye sifa kubwa ya kuwa na kasi ya 4G



Habari za chini ya kapeti zinasema kwamba simu hiyo ndiyo itakayokua ya bei nafuu sana kwenye soko katika kundi la simu zenye uwezo wa 4G na screen kubwa ya 6.6” inch na battery kubwa lenye uwezo wa 5000mAh ambalo unaweza kutumia kucheza micheo na kuangalia video mtandaoni kwa muda mrefu bila kuwa na wasi wasi wa kuishiwa chaji

Usanifu wa hali ya juu sio kitu unachokiona kwenye simu za Android ndani ya bajeti hii

Simu hii inawalenga sana vijana wa vyuoni, mama lishe, wamachinga, na wale watu ambao bajeti zao haziko vizuri na wangetamani kupata simu yenye uwezo bora zaidi katika matumizi.



Pia simu inasifiwa kwa kuwa na muonekano wenye kuvutia na pia mteja ataweza chagua simu katika rangi tatu zinazokuja na simu. Si hivyo tu, pia simu ina kuja na ofa kem kem kam bando la mwaka mzima la Vodacom la GB 60 na mazawadi ya kutosha .



Itel wanasema ukae mbali, maan wameazimia kuakikisha kila mtanzania mwenye ndoto ya kumiliki simu janja yenye uwezo mkubwa na sifa kibao ila bajeti ni ndogo basi A60 ndo itakua jibu la swali lao

Kwa taarifa Zaidi kujua nilini simu itaachiwa na Habari kamili tembelea kara sa zao za Facebook itel Tanzania au boya link kutembela kurasa yao ya Instagram https:/www.instagram.com/iteltanzania.

Post a Comment

0 Comments