Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS DKT. MWINYI AZINDUA NGUMI ZA KULIPWA ZANZIBAR VIWANJA VYA MAO ZEDUNG ZANZIBAR.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizindua Ngumi za Kulipwa Zanzibar katika Uwanja wa Mao Zedung Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar, jana usiku na (kushoto kwa Rais) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi na (kulia kwa Rais) Waziri wa Habari,Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe.Tabia Maulid Mwita na Naibu Waziri wa Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma.(Picha na Ikulu)
WAPENZI wa michezo Zanzibar wakiwa katika Uwanja wa Mao Zedung Wilaya ya Mjini Unguja, wakishuhudia uzinduzi wa Ndumi za Kulipwa Zanzibar, wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akizundua Mcezo wa Ngumi za Kulipwa Zanzibar jana usiku 27-8-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kuzindua Mchezo wa Ngumi za Kulipwa Zanzibar, uzinduzi huo uliofanyika katika Uwanja wa Mao Zedung Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar jana usiku 27-8-2023.(Picha na Ikulu)
MCHEZO wa Uzinduzi wa Ngumi za Kulipwa Zanzibar (Vitasa)kati ya Karimu Mandonga na Muller Junior uliofanyika jana usiku 27-8-2023 katika Uwanja wa Mao Zedung Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar, baada ya kuzinduliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, katika mchezo huo Bondia Muller Junior ameshinda.(Picha na Ikulu)

MSHANII wa Muziki wa Kizazi kipya Bongo Flava Ali Kiba akifuatilia mchezo wa ufunguzi wa Ngumi za Kulipwa Zanzibar (Vitasa ) kati ya Karimu Mandonga na Muller Junior, baada ya kuzinduliwa ngumi za kulipwa Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza lac Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi jana usiku 27-8-2023, katika uwanja wa Maon Zedung Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)


Post a Comment

0 Comments