Ticker

6/recent/ticker-posts

Benki ya NBC Yashirikiana Taasisi Sita Kuongeza Ukusanyaji Wa Mapato Zanzibar

Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesaini hati ya Makubaliano (MOU) na taasisi sita za Serikali ya Mapinduzi Zanzbar (SMZ) yanayotoa fursa kwa benki hiyo kutumika kukusanya malipo mbalimbali ya Serikali kupitia mtandao na mfumo na wa kidijitali wa benki hiyo.

Makubaliano hayo yanayohusisha Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA), Mfuko wa Hifadhi Jamii Zanzibar (ZSSF), Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS), Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO), Idara ya Ushirikiano wa Umma na Sekta Binafsi- Zanzibar (ZPPP) na Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) yanatajwa kuwa mbali na kurahisiha huduma ya malipo kwa wananchi pia yatasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuzuia upotevu wa mapato ya serikali.

Hafla ya utiaji Saini makubaliano hayo imefanyika hii leo Zanzibar ikiongozwa na Waziri Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango -Zanzibar Bi Saada Mkuya huku ikihusisha uwepo wa viongozi waandamizi wa mashirika hayo pamoja na maofisa wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi.

Akizungumzia kwenye hafla hiyo, Bi Mkuya pamoja na kuwapongeza wadau hao kwa ushirikiano huo alisema hatua hiyo inakwenda sambamba na adhima ya serikali ya SMZ kuelekea kukamilisha mfumo wake wa Serikali mtandao.

“Hatua hii ya leo kwa kiasi kikubwa inaunga mkono jitihada za serikali kutumia vizuri teknolojia na mifumo ya kielektroniki katika shughuli zake hususani katika ukusanyaji wa mapato. Hatua hii inatusaidia katika kurahisisha huduma za malipo mbalimbali kwa wananchi, kuongeza kasi na ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya serikali na zaidi pia kuzia mianya ya upotevu wa mapato ya serikali...tunawapongeza sana NBC na wadau wote kwa hatua hii,’’ alipongeza.

Kwa mujibu wa Bi Mkuya kupitia makubaliano hayo yanayohusisha taasisi kubwa za serikali ya SMZ, wananchi watanufaika moja kwa moja kupitia faida mbali mbali za kiuchumi na kijamii huku pia akibainisha kuwa mfumo utasaidia kuchochea suala zima la utawala bora kupitia uwazi katika ukusanyaji wa mapato ya serikali.

Awali akizungumza kwenye hafla hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi alisema ushirikiano huo ni muendelezo wa makubaliano ya awali ambayo kwa kiasi kikubwa yanaonyesha dhamira thabiti ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika kuboresha ufanisi wa ukusanyaji wa mapato yake kupitia mfumo wa Kielektroniki yaani (GEPG) au ZanMalipo.

“Kupitia makubaliano haya wananchi sasa wataweza kutumia mtandao wa Benki ya NBC kufanya malipo ya Serikali na ankara mbalimbali kupitia mtandao wa Benki ya NBC.’’

‘’Malipo hayo yanaweza kufanyika kupitia matawi yetu mawili yaliyopo hapa Zanzibar na pia kupitia zaidi ya mawakala wetu 207 waliopo kila kona ya Unguja na Pemba na pia kupitia huduma zetu za kidijitali yaani huduma za benki kwa njia simu (NBC Kiganjani ) na huduma zetu kupitia mtandao.’’ Alitaja.

Wakijadili kuhusu ushirikiano huo Kamishna Mkuu wa ZRA Yusuph Mwenda, Mkurugenzi Mkuu wa ZBS Yusuph Majid Nassor, Kamishna wa ZPPP Dkt. Bill Kiwia na Meneja wa Fedha ZECO Bi Riziki Faqih walitaja ushirikiano huo kama nyezo muhimu sio tu katika kukusanya mapato na kuongeza urahisi wa kusimamia mchakato wa kifedha bali pia ni kichocheo kikubwa cha maendeleo ya kiuchumi Zanzibar.

“Kupitia mfumo huu ni wazi kwamba tunakwenda kushuhudia ongezeko kubwa la mapato yetu kwa kuwa utasaidia sana kwanza kuondoa usumbufu uliokuwa unawakabili wananchi wengi kutembelea ofisi mbalimbali ili tu kufanya malipo mbalimbali ya serikali ikiwemo kodi na tozo za mamlaka za serikali na pia itachochea kasi ya malipo hayo kwa kuwa wananchi watatimiza wajibu huo kwa wingi wao kwa kuzingatia kwamba benki ya NBC ina mifumo rahisi nay a kisasa zaidi,’’ alisema.

Waziri Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Bi Saada Mkuya (katikati waliosimama) akiwashuhudia Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kushoto -walioketi) na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA) Yusuph Mwenda (Kulia – walioketi) wakitia Saini makubaliano yanayotoa fursa kwa benki hiyo kutumika kukusanya malipo mbalimbali ya Serikali ya SMZ kupitia mtandao na mfumo na wa kidijitali wa benki hiyo. Hafla ya utiaji Saini makubaliano hayo imefanyika hii leo Zanzibar ikiongozwa na Mkuya.
Waziri Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Bi Saada Mkuya (katikati waliosimama) akiwashuhudia Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kushoto -walioketi) na Kamishna wa Idara ya Ushirikiano wa Umma na Sekta Binafsi- Zanzibar (ZPPP) Dkt. Bill Kiwia (Kulia – walioketi) wakitia Saini makubaliano yanayotoa fursa kwa benki hiyo kutumika kukusanya malipo mbalimbali ya Serikali ya SMZ kupitia mtandao na mfumo na wa kidijitali wa benki hiyo. Hafla ya utiaji Saini makubaliano hayo imefanyika hii leo Zanzibar ikiongozwa na Mkuya.
Waziri Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Bi Saada Mkuya (katikati) akiwashuhudia Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS) Yusuph Majid Nassor, (wa pili Kulia) wakibadilishana hati za makubaliano yanayotoa fursa kwa benki ya NBc kutumika kukusanya malipo mbalimbali ya Serikali ya SMZ kupitia mtandao na mfumo na wa kidijitali wa benki hiyo. Hafla ya utiaji Saini makubaliano hayo imefanyika hii leo Zanzibar ikiongozwa na Mkuya.
Waziri Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Bi Saada Mkuya (katikati) akiwashuhudia Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (wa pili kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) Vuai Yahya Lada (Kushoto) wakibadilishana hati za makubaliano yanayotoa fursa kwa benki ya NBc kutumika kukusanya malipo mbalimbali ya Serikali ya SMZ kupitia mtandao na mfumo na wa kidijitali wa benki hiyo. Hafla ya utiaji Saini makubaliano hayo imefanyika hii leo Zanzibar ikiongozwa na Mkuya.
Makubaliano hayo yanayohusisha Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA), Mfuko wa Hifadhi Jamii Zanzibar (ZSSF), Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS), Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO), Idara ya Ushirikiano wa Umma na Sekta Binafsi- Zanzibar (ZPPP) na Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) yanatajwa kuwa mbali na kurahisiha huduma ya malipo kwa wananchi pia yatasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuzuia upotevu wa mapato ya serikali.

Akizungumzia kwenye hafla hiyo, Waziri Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango -Zanzibar Bi Saada Mkuya (pichani) pamoja na kuwapongeza wadau hao kwa ushirikiano huo alisema hatua hiyo inakwenda sambamba na adhima ya serikali ya SMZ kuelekea kukamilisha mfumo wake wa Serikali mtandao

Awali akizungumza kwenye hafla hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (pichani) alisema ushirikiano huo ni muendelezo wa makubaliano ya awali ambayo kwa kiasi kikubwa yanaonyesha dhamira thabiti ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika kuboresha ufanisi wa ukusanyaji wa mapato yake kupitia mfumo wa Kielektroniki yaani (GEPG) au ZanMalipo.


Wakijadili kuhusu ushirikiano huo Kamishna Mkuu wa ZRA Yusuph Mwenda (alieshika kipaza sauti) Mkurugenzi Mkuu wa ZBS Yusuph Majid Nassor (wa pili kulia) Kamishna wa ZPPP Dkt. Bill Kiwia (kushoto) na Meneja wa Fedha ZECO Bi Riziki Faqih (Kulia) walitaja ushirikiano huo kama nyezo muhimu sio tu katika kukusanya mapato na kuongeza urahisi wa kusimamia mchakato wa kifedha bali pia ni kichocheo kikubwa cha maendeleo ya kiuchumi Zanzibar.

Hafla ya utiaji Saini makubaliano hayo imefanyika hii leo Zanzibar ikiongozwa na Waziri Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango -Zanzibar Bi Saada Mkuya (Katikati) huku ikihusisha uwepo wa viongozi waandamizi wa mashirika hayo pamoja na maofisa wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (wa pili kulia)
Waziri Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango -Zanzibar Bi Saada Mkuya (Kulia -walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya maofisa wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi (kushoto) wakati wa hafla hiyo.

Post a Comment

0 Comments