Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS DKT. MWINYI AWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA VIWANJA VYA NJE YA UWANJA WA AMAAN ZANZIBAR

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiondoa pazia kuweka Jiwe la Msingi wa ujenzi wa Viwanja vya nje ya Uwanja wa Amaan Zanzibar  (kushoto) Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya ORKUN inayojenga Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar. Bw. Ilhan Karadeniz, hafla hiyo iliyofanyika jana usiku 14-12-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi  akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla na Viongozi mbalimbali, alipowasili katika Uwanja wa Amaan  kwa ajili ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la ujenzi  wa viwanja vya nje ya Uwanja wa Amaan Zanzibar, hafla hiyo iliyofanyika jana usiku 14-12-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zuberi Ali Maulid, wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya ORKUN inayojenga uwanja huo Bw. Ilhan Karadeniz, wakati akitembelea Viwanja vya Nje ya Uwanja wa Amaan Zanzibar baada ya kuweka Jiwe la Msingi la ujenzi huo, hafla hiyo iliyofanyika jana usiku 14-12-2023.(Picha na Ikulu)
BAADHI ya Wafanyakazi wa Kampuni ya ORKUN inayojenga Uwanja wa Amaan Zanzibar na Wananchi wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia katika hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Viwanja vya Nje ya Uwanja wa Amaan Zanzibar, hafla hiyo iliyofanyika jana usiku 14-12-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwasalimia na kuwapongeza  Wanafunzi wa Skuli ya Jangombe Unguja Fadhila Ibrahim na Sharifa Somea, baada ya kumaliza kutowa burudani ya Ngoma ya Kunguwia, wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Viwanja vya Nje ya Uwanja wa Amaan Zanzibar iliyofanyika jana usiku 14-12-2023.(Picha na Ikulu)
WATOTO wa Kikundi cha Mchezo wa Karate cha Island Warriors  Zanzibar wakionesha umahiri wa mchezo huo wakati wa uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Viwanja vya Nje ya Uwanja wa Amaan Zanzibar, hafla hiyo iliyofanyika jana usiku 14-12-2023.(Picha na Ikulu)

Post a Comment

0 Comments