Msanii wa Mziki wa Bongo fleva nchini Michael Muganda (Mycoely) amesaini hati ya makubaliano na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ya kuwa Balozi wa Mazingira nchini.
Hati hiyo ya makubaliano imesainiwa Julai 11, 2026 kwenye Maadhimisho ya Siku ya Mazingira kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba).
Akizungumza mara baada ya zoezi hilo, Mycoely amesema amepokea kwa furaha kubwa na jukumu lake ni moja tu kuhakikisha anafikisha ujumbe wa umuhimu wa kutunza Mazingira kwa Watanzania.











0 Comments