Ticker

6/recent/ticker-posts

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI YATEMBELEA BODI YA MFUKO WA BARABARA


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali Mhe. Naghenjwa Kaboyoka (Mb.) akipokea matangazo ya Mfumo wa Kielektroniki ya Ufuatiliaji wa Hali ya Barabara kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Barabara Octavian Mshiu (Kulia), wanaoshuhudia ni Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Ujenzi) Balozi Mhandisi Aisha Amour pamoja na Meneja wa Mfuko wa Barabara Eliud Nyauhenga (Kushoto).

Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Ujenzi) Balozi Mhandisi Aisha Amour, akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali wakati kamati hiyo ilipotembelea Ofisi za Bodi ya Mfuko wa Barabara jijini Dodoma kwa ajili ya kujifunza utendaji kazi wa Bodi hiyo, kushoto kwake ni Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Naghenjwa Kaboyoka (Mb.) na kulia kwake ni Meneja wa Mfuko wa Barabara Eliud Nyauhenga.


Meneja wa Mfuko wa Barabara Eliud Nyauhenga, akifanua jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali wakati kamati hiyo ilipotembelea Ofisi za Bodi ya Mfuko wa Barabara jijini Dodoma kwa ajili ya kujifunza utendaji kazi wa Bodi hiyo.


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali Mhe. Naghenjwa Kaboyoka (Mb.) akielekeza jambo wakati kamati hiyo ilipotembelea Ofisi za Bodi ya Mfuko wa Barabara jijini Dodoma kwa ajili ya kujifunza utendaji kazi wa Bodi hiyo, kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Barabara Octavian Mshiu.


Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali Mhe. Anton Mwantona (Mb.) akiuliza swali wakati kamati hiyo ilipotembelea Ofisi za Bodi ya Mfuko wa Barabara jijini Dodoma kwa ajili ya kujifunza utendaji kazi wa Bodi hiyo.

Post a Comment

0 Comments